Tuesday 17 September 2013

LICHA ya adha wanayoipata wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (albino) wanaoishi shule maalumu ya Bughangija iliyopo manispaa ya Shinyanga ikiwemo uhaba wa chakula, matibabu pamoja na makazi bora lakini bado wazazi na walezi wa watoto hao hawana njia ya kulinda usalama wao zaidi ya kuendelea kuwapeleka shuleni hapo.

Watoto hawa (Pichani) wakiwa na wazazi wao wakiingia shuleni hapo juzi na kuongeza idadi ya wanafunzi waliopo shuleni hapo zaidi 100 waliolazimika kutengana na familia zao kutokana na kuibuka kwa wimbi la mauaji ya walemavu wa ngozi nchini hususani katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita na Tabora.

No comments:

Post a Comment